Browsing by Author "wizara ya kilimo"
Now showing 1 - 4 of 4
Results Per Page
Sort Options
Item Halmashauri ya taifa ya mazao(Nuta Press, 1971) wizara ya kilimoKabla ya Tanzania kupata uhuru, serikaii ya kikoloni ilijiingiza sana katika mazao ya biashara na nchi za nje na haikujali sanajuu ya mazao yaliyotumika humu nchini hasa yale ya chakula ambayo wananchi hutumia. Siasa yao ya kikoloni wakati huo ilikuwa kuku- za mazao ambayo yangeuzwa na kukuza uchumi wa nchi zao. Siasa hiyo kwa kweli iliweza kuleta madhara kwa mazao ambayo yangetumika au kuliwa humu nchini, kwa hiyo upanuzi wa kilimo cha mazao machache kuliifanya Tanganyika kutesemea mazao kama katani na kahawa kuwa mazao makuu ya biashara na nchi za nje.Item Karanga(Sokoine university of agriculture, 1987) wizara ya kilimoKaranga ni zao zuri sana ambalo hutumika kama chakula na mafuta pia,karanga hupandwa sehemu tofauti nchini Tanzania.karanga hupandwa kwa kufuata kanuni zifuatazo kabla ya kupanda, chagua mbegu ambazo hazishambuliwi na wadudu au magonjwa, ondoa mbegu zilizo sinyaa na kutupa mbali kabla ya kupanda.Item Kilimo bora cha mbono(Jatropha(Sokoine university of agriculture, 2023-11-18) wizara ya kilimoMmbono kwa kitaalam Jatropha curcas ni mti jamii ya nyonyo wenye mbegu zitoazo mafuta yenye sifa kama nyonyo.Huota kwenye maeneo ya nyanda kame na yenye upungufu wa rutuba. Mmea hauliwi na mifugo wala wanyama pori na kufanya mmea ufae kulimwa kwenye maeneo ya wafugaji huria. Mmea hutoa mbegu zenye mafuta ambayo hayaliwi bali hutengenezea sabuni, kuendesha mitambo, gesi kama nishati.Kutokana na faida nyingi kwa binadamu kiafya, kiuchumi na mazingira, mmea unaweza kuzalishwa kama zao. Mmea huu umetokea Marekani ya Kati na kusambazwa hadi Afrika Mashariki na Wareno.Item Wakulima wa pamba(Sokoine university of agriculture, 2023-12-01) wizara ya kilimoWakulima wa pamba ni wadau wakuu katika sekta ndogo ya pamba huku mchango wao ndio unaotegemewa zaidi kuiinua tasnia ya pamba. Pamba inalimwa na wakulima wadogo wenye mashamba ya ukubwa wa kuanzia ekari 1 hadi ekari 10.Sehemu kubwa ya wakulima hutumia jembe la kokotwa na wanyama kazi na jembe la mkono huku sehemu ndogo wakitumia trekta kuandaa mashamba.