Ghala la Taarifa na machapisho ya kilimo
Ghala hili,limebeba machapisho na taarifa mbalimbali za kilimo zilizo rahisishwa kwa matumizi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, maafisa ugani na wadau wengine wa kilimo.

Recent Submissions
Kanuni na teknolojia bora za uzalishaji na usimamizi wa zao la bamia baada ya kuvuna
(Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID), 2019-11) Wizara ya Kilimo Tanzania
Bamia ni zao linalolimwa katika maeneo mengi nchini kutokana na umuhimu wake kilishe na kuongeza kipato. Asili ya zao hili ni Afrika ya Magharibi lakini kwa sasa limeeenea katika nchi nyingi za ukanda wa kitropiki. Bamia ni zao lenye mchango katika afya ya mwanadamu na ni chanzo muhimu cha vitamini na madini ya potasiam na chokaa ambayo ni muhimu kwa afya ya mifupa, meno na husaidia ufanyaji kazi mzuri wa misuli. Wakulima walio wengi hususan wakulima wadogo, hutegemea zao hili kama chanzo cha kipato kutokana na kutumiwa na watanzania walio wengi.
Njia bora za kutekeleza na kukabiliana na mabadiliko tabia nchi katika thamani ya soko la nafaka
(Easter Africa Grain Council - EAGC, 2020) Baraza la Nafaka la Afrika Mashariki
Kuhakikisha uwepo wa chakula cha kutosha Afrika mashariki, IGAD na ICPAC wamekuwa wakifanya usimamizi wa uzalishaji wa mazao ya nafaka. EAGC kama mdau mkubwa wa ICPAC wamekuwa na mchango mkubwa katika kutoa taarifa za hali ya soko la mazao kupitia taasisi yake ya kikanda ya kilimo, biashara na usalama wa chakula ya (RATIN) kupitia machapisho yao, wadau wa ongezeko la thamani la nafaka wanapata taarifa za kila wiki, mwezi na msimu mzima kuhusiana na utabiri wa hali ya hewa na usalama wa chakula.
Uhifadhi wa malisho
(Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TAURI), 2023) Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania
Mavuno ya malisho katika sehemu za tropiki hutofautiana kwa wingi na ubora kutegemeana na aina, ukomavu, hali ya hewa rutuba ya udongo na matunzo. Majani na miti ya malisho yaliyovunwa huhifadhiwa ili kutumika wakati wa upungufu wa malisho kipindi cha kiangazi. Hifadhi ya malisho inaathiriwa na mabadiliko ya hali ya hewa, uzalishaji hafifu na uelewa mdogo wa mbinu za uhifadhi.
Kilimo cha mbaazi za muda mrefu
(Mradi wa IFAD, 2025) Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI)
Mbaazi ni zao la jamii kubwa ya mazao aina ya mikunde, faida zake kubwa ni chanzo cha viini lishe vya protini kwa binadamu na wanyama, linavumilia ukame, hupunguza umasikini kwani zao hili ni chanzo cha mapato kwa kaya, hurutubisha udongo kwani katika kilima kwake linaweza kuchanganywa na mazao mengine shambani kama vile mahindi na mtama.
Mabadiliko ya hali ya hewa Oktoba - Disemba 2026
(Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA), 2026-08-28) Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA)
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa mwelekeo na taarifa rasmi ya msimu wa mvua za Vuli (Oktoba hadi Desemba) 2026, ikionyesha kuwepo kwa mfumo wa hali ya hewa wa El NiƱo yenye nguvu kubwa.Wananchi washauriwa namna ya kuandaa mashamba, mazao ya kuzingatia na mbegu gani zitumike