Ghala la Taarifa na machapisho ya kilimo

Ghala hili,limebeba machapisho na taarifa mbalimbali za kilimo zilizo rahisishwa kwa matumizi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, maafisa ugani na wadau wengine wa kilimo.

Photo by @inspiredimages
 

Communities in DSpace

Select a community to browse its collections.

Now showing 1 - 1 of 1

Recent Submissions

Item
Lishe bora za mifugo kutoka Yara
(YARA, 2023) YARA
Kipeperushi hiki kinaelezea lishe bora za mifugo kutoka YARA, kinaongelea kuhusu Protini ya Ng'ombe, mbuzi na Kondoo ambayo inaitwa FEED GRADE UREA, vile vile ili kuboresha Afya na Utagaji wa Mayai kwa kuku utatumia KYIMOFOS 21 na ili kuongeza ladha na ulaji wa chakula kwa mifugo yako utatumia kalori 3000 na VARA FEED GRADE SULPHUR kwa Mifugo lliyonona na Kipato Kikubwa.
Item
Kituo cha Taifa cha uhimilishaji (NAIC)
(WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI, 2024) WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI
Uhimiishaji ni njia pekee ambayo inabadilisha uzao wo wanyama kwa haraka zaidi. Hii ina maanisha kwamba, kama mfugaji ana ng'ombe wa kienyeji ni rahisi kumtungisha mimba ya dume wa kisasa wa aina inayofaa kwenye eneo lake na hivyo kupata chotara ambaye atayamudu mazingira husika. Ni njia sahihi ya kuzuia kuenea kwa magonjwa ya kizazi kama vile Ugonjwa wa kutupa mimba (Brucellosis)., Vibriosis, Leptospirosis na Trichomoniasis. Magonjwa haya yanaenezwa kwa ngo’mbe dume aliyeathirika kumpanda ng’ombe jike. Magonjwa haya huleta hasara kubwa kwa wafugaji hasa ya kukosa uzao wa ng’ombe kwa wakati uliotarajiwa. Mfugaji anaepuka gharama na hatari za kufuga madume. Madume wa ng'ombe wa kisasa huwa ni wakali na wakubwa, wanahitaji malishao mengi na uangalifu mkubwa wakati wa kumfuga. Kurahlsisha uchaguzi wa dume linalotakiwa kuwekwa kama dume la mbegu. Kwa kutumia njia ya uzalishaji kwa chupa wazalishaji (breeders) wanarahisishiwa kumchagua dume (replacement bull) kwa sababu mbegu za madume zinakuwa zimeshatumika kwa ngombe wengi kuliko kwa kutumia njia ya kawaida.
Item
Kilimo bora cha alizeti
(TARI, 2025) Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI)
Zao la alizeti ni miongoni mwa mazao ya mbegu za mafuta, zao hili hutoa mafuta ya kula kwa binadamu na mashudu kwa ajili ya chakula cha mifugo. Alizeti ni zao lenye thamani kiuchumi na mafuta hutumika katika utengenezaji wa vipodozi, madawa na nishati mbadala kwenye viwanda maua ya alizeti hutumika kama mapambo na kutoa chavua kwa ajili ya nyuki kutengeneza asali huongeza tija ya uzalishaji wa alizeti inashauriwa kufuata maelekezo ya kipeperushi hiki na mwongozo na kalenda ya kilimo bora cha alizeti uliotolewa na Wizara ya Kilimo mwaka 2022.
Item
Utaratibu wa kumwagilia maji kwa teknologia ya AWD
(Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), 2023) Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI)
Usimamizi wa maji ni mojawapo ya shughuli muhimu katika kilimo cha mpunga Inashauriwa kumwagilia kwa mfumo wa kuingiza na kusubili maji yakauke shambani kabla ya kumwagilia tena (AWD). Kwa kufanya hivyo husaidia kupunguza maji kati ya asilimia 40-50 kuanzia hatua ya kupanda hadi kuvuna. Mbinu hii, husaidia mzunguko wa hewa ardhini katika mashamba ya mpunga na pia inasaidia mizizi kukuwa vizuri.
Item
Dhibiti ugonjwa wa Ubwiri unga wa Mikorosho kwa kutumia kiuatilifu cha maji.
(TARI, 2025) TARI
Moja ya matatizo makubwa ya uzalishaji wa zaola korosho ni ugonjwa wa Ubwiri unga, ambaoumeenea katika mikoa yote Tanzania. Ugonjwa huo husababishwa na vimelea aina ya kuvu nahuweza kupunguza mavuno kwa zaidi ya asilimia 70.