Ghala la Taarifa na machapisho ya kilimo
Ghala hili,limebeba machapisho na taarifa mbalimbali za kilimo zilizo rahisishwa kwa matumizi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, maafisa ugani na wadau wengine wa kilimo.

Recent Submissions
Usajili wa aina mpya za mbegu za mimea ya mazao
(TOSCI, 2017) Taasisi ya kudhibiti ubora wa mbegu Tanzani (TOSCI)
Utaratibu wa Kusajili Aina Mpya za Mbegu. Kanuni ya 7 ya mbegu inataka kila aina mpya ya mbegu itakayosajiliwa nchini ifanyiwe majaribio ya Utambuzi (DUS Test) na Umahiri (NPT) isipokua kwa aina za mboga mboga ambazo husajiiwa baada ya kufanya jaribio la utambuzi tu. Pia Kanuni ya mbegu (4(2)) inaruhusu Tanzania kupokea taarifa ya majaribio ya Utambuzi kutoka nchi wanachama wa UPOV.
Jarida la Mifugo na Uvuvi
(Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025-04) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Serikali imekuwa ikichukua hatua na kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukabiliana na uvuvi haramu. Mikakati hiyo ni pamoja na kufanya maboresho ya Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo inayosimamia rasilimali za uvuvi ikiwemo matumizi ya teknolojia za kisasa katika kusimamia rasilimali za uvuvi, kuimarisha Vikundi vya Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi (BMUs), kutoa elimu ya kudhibiti uvuvi haramu na matumizi endelevu ya rasilimali za uvuvi, kuhamasisha uanzishwaji wa Vyama vya Ushirika wa Wavuvi na kuimarisha ufugaji wa viumbe maji.
Jinsi ya kutambua mbegu zisizo na ubora na mbegu bandia (FEKI )
(TOSCI, 2017) Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu
Matumizi ya mbegu zisizo na ubora na mbegu bandia (feki) yamesababisha wakulima kupoteza kipato kwa kupata mazao hafifu na hata kutopata mavuno kabisa. Sheria ya Mbegu ya Mwaka 2003, inamlinda mkulima asiuziwe mbegu zisizo na ubora na mbegu bandia (feki). Pamoja na kuthibitisha ubora wa mbegu, TOSCI ina jukumu la kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo ili kumlinda rnkulima asiuziwe mbegu zisizo na ubora na mbegu feki.
Jarida la Mifugo na Uvuvi
(Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025-02) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
UVUVI NI UTAJIRI! ndivyo ambavyo unaweza kusema kupitia Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo inahakikisha inaleta mapinduzi makubwa katika Sekta ya Uvuvi kwa kuweka jicho la kipekee kwenye Uchumi wa Buluu. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatekeleza mradi wa ukopeshaji wa boti za kisasa kwa wavuvi wa Ukanda wa Pwani, Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa, ambapo mradi huo unalenga kuwezesha wananchi kufanya uvuvi na ukuzaji viumbe maji endelevu na wenye tija na kuwajengea mazingira wezeshi ili waweze kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi.
Jarida maalum la nanenane
(Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Wizara ya mifugo na uvuvi imeibuka na ushindi huo baada ya kuongoza katika vigezo mbalimbali hali iliyochagizwa na maandalizi mazuri iliyofanya katika maonesho hayo huku kivutio kikubwa kikiwa ni Paredi ya Mifugo iliyoambatana na maonesho ya Ndege nyuki maalum inayotumika kwenye udhibiti wa Uvuvi haramu. Akizungumza katika kilele cha Maonesho hayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mbali na kuipongeza Wizara hiyo kwa jitihada ilizochukua katika udhibiti wa magonjwa ya Mifugo kupitia utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo, ameielekeza kuhakikisha inaweka kituo cha Ugani kwenye viwanja vya Maonesho hayo jijini Dodoma ambavyo rasmi leo vimetambulishwa kwa jina la Dkt. John Samwel Malecela ili wananchi
waendelee kunufaika na elimu ya masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Mifugo na Uvuvi