Ghala la Taarifa na machapisho ya kilimo

Ghala hili,limebeba machapisho na taarifa mbalimbali za kilimo zilizo rahisishwa kwa matumizi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, maafisa ugani na wadau wengine wa kilimo.

Photo by @inspiredimages
 

Communities in DSpace

Select a community to browse its collections.

Now showing 1 - 1 of 1

Recent Submissions

Item
Usindikaji rahisi wa muhogo
(Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo( SUA ), 2022) Silayo V. C. K.; Laswai H. S.; Mpagalile J. J.; Ballegu W. R.; Makungu P. J.; Mtunda K.; Chilosa D.; Nyborg I.
Muhogo ni zao mbadala kwa wakulima wa "Tanzania. Faida za muhogo ni nyingi na hasa katika kuongeza uhakika wa chakula na pato la kaya. Uboreshwaji wa njia za kusindika muhogo ili kupata aina mbalimbali za vyakula umeongeza nafasi ya muhogo katika kilimo hapa Tanzania. Shime sote tuongeze juhudi katika kilimo cha muhogo - MUHOGO NI MALI.
Item
Zijue taratibu za uzalishaji wa mbegu za viazi vitamu zilizothibitishwa ubora wake
(Mradi wa Bioinnovate - ICOPSEA, 0209-07) Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Mikocheni
Viazi vitamu ni zao muhimu la chakula na lishe bora nchini Tanzania. Viazi vitamu vina wanga mwingi hivyo ni njia nafuu ya kuupatia mwili nguvu. Majani ya viazi vitamu hutumika kama mboga na hivyo ni chanzo cha vitamini na madini joto mwilini. Pia viazi vitamu ni chanzo cha kipato kwa familia na taifa.
Item
Matunzo ya shamba na uvunaji wa zabibu
(TARI, 2024) Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania
MATUNZO YA SHAMBA NA UVUNAJI Ili kupata mavuno yenye tija ni muhimu kutunza vizuri shamba la mizabibu. Matunzo ya shamba ni pamoja na kupalilia, kutifulia, kudhibiti visumbufu na kukatia mizabibu.  Palilia shamba mara kwa mara ili kudhibiti magugu, kwa wastani palizi tatu zinatosha katika msimu mmoja .  Ni muhumu kutifulia udongo kwenye shamba la mizabibu kila wakati ili kuvuna maji ya mvua.
Item
Utayarishaji wa mboga za majani
(Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo(SUA ), 2015) Kinabo J. L.; Msuya J.M.; Mnkeni A.P.; Nyaruhucha C.; Ishengoma J.
Mboga za majani zinashika nafasi muhimu sana katika vyakula vyetu. Zinaliwa kila siku na mara nyingi zaidi ya mara moja kwa siku. Zipo aina nyingi za mboga za majani, nyingine zinalimwa na nyingine zinaota zenyewe porini na mashambani wakati wa msimu wa mvua. Mboga zina virutubishi kama madini na vitamini ambavyo vinahitajika mwilini kwa afya bora. Hata hivyo pamoja na kwamba zina virutubishi vya kutosha na zinaliwa kila siku, watu wengi wanapata matatizo ya afya yanayotokana na ukosefu wa virutubishi vinavyopatikana katika mboga za majani kwa mfano upofu na upungufu wa damu. Hali hii inajitokeza kwa sababu gani?
Item
Kilimo cha Pilipili Mtama
(Wizara ya kilimo na Chakula, Tanzania, 2022) Sehemu ya Uinuaji Mazao, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika
Pilipili mtama ni zao ambalo asili yake ni Mashariki ya Mbali, na linalimwa zaidi katika mkoa wa Tanga na Zanzibar. Matumizi Pilipili nyeusi na nyeupe zote hutumika kwa mapishi ya nyama, samaki na kwa mapishi mengine mbalimbali