Ghala la Taarifa na machapisho ya kilimo
Ghala hili,limebeba machapisho na taarifa mbalimbali za kilimo zilizo rahisishwa kwa matumizi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, maafisa ugani na wadau wengine wa kilimo.

Recent Submissions
Ufugaji bora wa samaki
(International Tanfeeds, 2023) Iternational Tanfeeds
MBINU MUHIMU WAKATI WA UANZISHAJI UFUGAJI WA SAMAKI
• Mfugaji anatakiwa awe na shauku na dhamira ya kweli ya ufugaji.
• Kufanya tathmini ya rasilimali alizonazo kwa ajili ya mradi wa ufugaji wa samaki.
• Chanzo endelevu cha mtaji kwa ajili ya mradi.
• Hulka ya uvumilivu na kuthubutu.
• Tathmini ya soko la bidhaa za samaki.
• kujipatia maarifa ya msingi ya ufugaji wa samaki
Jarida maalum la nane nane 2025
(Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango
amewataka viongozi wa sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi nchini kuifanya Tanzania
kuwa kitovu cha chakula katika ukanda wa Afrika.
Mhe. Dkt. Mpango amesema hayo wakati wa hotuba yake ya Ufunguzi wa Maonesho
ya kimataifa ya Nane Nane aliyoitoa Agosti 1, 2025 kwenye Viwanja vya Nzuguni jijini
Dodoma ambapo amesisitiza Viongozi hao kuwa kinara kwenye utekelezaji wa dira ya
Taifa Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025-2050.
Aidha Dkt. Mpango amewataka wafugaji kuwekeza katika uzalishaji wa kisasa wa
bidhaa zinazotokana na mifugo ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje, kuendeleza
uvuvi na ufugaji wa samaki na kuvutia wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza kwenye
miundombinu baridi ya uhifadhi na usafirishaji wa mazao wa Mifugo na Uvuvi.
Ufugaji bora wa samaki 2025
(International Tanfeeds LTD, 2025) International Tanfeeds
MBINU MUHIMU WAKATI WA UANZISHAJI UFUGAJI WA SAMAKI
Mfugaji anatakiwa awe na shauku na dhamira ya kweli ya ufugaji.
Kufanya tathmini ya rasilimali alizonazo kwa ajili ya mradi wa ufugaji wa samaki.
Chanzo endelevu cha mtaji kwa ajili ya mradi.
Hulka ya uvumilivu na kuthubutu.
Tathmini ya soko la bidhaa za samaki.
kujipatia maarifa ya msingi ya ufugaji wa samaki
Tambua sifa za mbegu bora za viazi mviringo
(TARI, 2025) TARI
Viazi mviringo ni zao muhimu la chakula na
biashara ambalo idadi ya wahitaji inaongezeka
kila siku nchini Tanzania. Hapa nchini viazi
hustawi vizuri zaidi sehemu za miinuko zenye
mvua nyingi na baridi kali
Kilimo cha viazi vitamu - Tanzania
(Kituo cha Utafiti wa Miwa Kibaha, 2024) Kituo cha Utafiti wa Miwa Kibaha
Viazi vitamu ni zao mojawapo muhimu la
chakula na lishe bora nchini Tanzania. Viazi
vitamu vina wanga mwingi hivyo ni njia rahisi
ya kuupatia mwili nguvu. Majani ya viazi
vitamu yanatumika kama mboga na kuupatia
mwili vitamini na madini. Pia viazi vitamu
ni chanzo cha kipato. Hata hivyo, wastani wa
uzalishaji shambani ni mdogo kiasi cha 5.6t/ha
ukilinganisha na uzalishaji unaoweza kufikiwa
wa 20–40t/ha. Soko la viazi vitamu sio maalum,
kuna wauzaji wadogo na wakubwa.