Ghala la Taarifa na machapisho ya kilimo
Ghala hili,limebeba machapisho na taarifa mbalimbali za kilimo zilizo rahisishwa kwa matumizi ya wakulima, wafugaji, wavuvi, maafisa ugani na wadau wengine wa kilimo.

Recent Submissions
Usindikaji rahisi wa muhogo
(Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo( SUA ), 2022) Silayo V. C. K.; Laswai H. S.; Mpagalile J. J.; Ballegu W. R.; Makungu P. J.; Mtunda K.; Chilosa D.; Nyborg I.
Muhogo ni zao mbadala kwa wakulima wa
"Tanzania. Faida za muhogo ni nyingi na
hasa katika kuongeza uhakika wa chakula
na pato la kaya. Uboreshwaji wa njia za
kusindika muhogo ili kupata aina mbalimbali
za vyakula umeongeza nafasi ya muhogo
katika kilimo hapa Tanzania. Shime sote
tuongeze juhudi katika kilimo cha muhogo -
MUHOGO NI MALI.
Zijue taratibu za uzalishaji wa mbegu za viazi vitamu zilizothibitishwa ubora wake
(Mradi wa Bioinnovate - ICOPSEA, 0209-07) Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Mikocheni
Viazi vitamu ni zao muhimu la chakula na lishe bora nchini Tanzania. Viazi vitamu vina
wanga mwingi hivyo ni njia nafuu ya kuupatia mwili nguvu. Majani ya viazi vitamu
hutumika kama mboga na hivyo ni chanzo cha vitamini na madini joto mwilini. Pia viazi
vitamu ni chanzo cha kipato kwa familia na taifa.
Matunzo ya shamba na uvunaji wa zabibu
(TARI, 2024) Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania
MATUNZO YA SHAMBA NA UVUNAJI
Ili kupata mavuno yenye tija ni muhimu
kutunza vizuri shamba la mizabibu. Matunzo ya
shamba ni pamoja na kupalilia, kutifulia,
kudhibiti visumbufu na kukatia mizabibu.
Palilia shamba mara kwa mara ili
kudhibiti magugu, kwa wastani palizi tatu zinatosha katika msimu mmoja .
Ni muhumu kutifulia udongo kwenye shamba la mizabibu kila wakati ili
kuvuna maji ya mvua.
Utayarishaji wa mboga za majani
(Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo(SUA ), 2015) Kinabo J. L.; Msuya J.M.; Mnkeni A.P.; Nyaruhucha C.; Ishengoma J.
Mboga za majani zinashika nafasi muhimu
sana katika vyakula vyetu. Zinaliwa kila siku
na mara nyingi zaidi ya mara moja kwa
siku. Zipo aina nyingi za mboga za majani,
nyingine zinalimwa na nyingine zinaota
zenyewe porini na mashambani wakati wa
msimu wa mvua. Mboga zina virutubishi
kama madini na vitamini ambavyo
vinahitajika mwilini kwa afya bora. Hata
hivyo pamoja na kwamba zina virutubishi
vya kutosha na zinaliwa kila siku, watu
wengi wanapata matatizo ya afya
yanayotokana na ukosefu wa
virutubishi
vinavyopatikana katika mboga za majani
kwa mfano upofu na upungufu wa damu.
Hali hii inajitokeza kwa sababu gani?
Kilimo cha Pilipili Mtama
(Wizara ya kilimo na Chakula, Tanzania, 2022) Sehemu ya Uinuaji Mazao, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika
Pilipili mtama ni zao ambalo asili yake ni Mashariki ya Mbali, na linalimwa zaidi katika mkoa wa Tanga na Zanzibar. Matumizi Pilipili nyeusi na nyeupe zote hutumika kwa mapishi ya nyama, samaki na kwa mapishi mengine mbalimbali