UENDELEZAJI WA VIKUNDI VYA WAKULIMA KANDA YA MASHARIKI - Warsha ya Nane ya Wakulima wa Kanda ya Mashariki Iliyofanyika Ukumbi wa CCM, Lushoto, Tanga - 21-23 Juni 2004

Loading...
Thumbnail Image

Date

2005

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

TARP II-SUA Project

Abstract

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo na Chakula (MAFS), na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Norway (NLH), kinatekeleza mradi wa Utafiti wa Uhakika wa Chakula na Pato la Kaya kwa Wakulima Wadogowadogo Tanzania. Mradi huu ambao ulianza rasmi mwezi Septemba 2000, unagharamiwa na Serikali ya Norway. Kati ya shughuli muhimu zilizopangwa ili kutekeleza malengo ya mradi na kuimarisha uhusiano na wakulima, watafiti na washauri wa wakulima ni kufanya warsha zenye madhumuni yafuatayo: • Kuwajumuisha watafiti, wakulima na washauri wa kilimo ili kudadisi kuhusu mambo muhimu yanayohitaji kushirikishwa pande zote kwa lengo la kufanikisha kilimo na ufugaji • Kuchambua na kuainisha matatizo yanayowakabili wakulima wadogowadogo • Kupanga ili kutambua mambo gani yapewe uzito au kipaumbele • Kushiriki katika kupeana uzoefu wa maeneo muhimu ya kilimo na mifugo. Chapisho hili linawasilisha mwenendo wa Warsha ya nane ya wakulima wa Mikoa ya kanda ya Mashariki kuhusu Uendelezaji wa Vikundi vya Wakulima iliyofanyika ukumbi wa CCM, Lushoto, Tanga, 21-23, Juni 2004. Mwenendo wa warsha umechapishwa na kutolewa katika lugha ya Kiswahili na Kiingereza.

Description

Keywords

Ushirika, Vikundi

Citation

Collections