Uzalishaji Mazao
Permanent URI for this collection
Browse
Recent Submissions
Item Kilimo Bila Udongo(Globalpublishers.co.tz, 2020-01) Globalpublishers, Globalpublisherskilimo Bila Udongo,katika teknolojia hii, kinachofanyika ni kujua ili mmea uweze kumea, kukua na kutoa mazao, huwa unahitaji virutubisho na madini gani katika ardhi? Ukishajua mahitaji hayo, basi zinatafutwa kemikali zenye virutubisho vinavyotakiwa, zinachanganywa kwenye maji na kuwekwa kwenye mabomba maalum ambayo kwa juu, huwa yana matundu maalum ambapo ndipo mmea unaotakiwa kulimwa,/huwekwa.Item Kilimo cha Nyanya Chungu(Mjasiriamali Hodari, 2018-02)Nyanya chungu ni zao jamii ya mbogamboga linalotumika kwa matumizi mengi kama mboga, dawa n.k. Zao hili hustawi maeneo yenye halijoto tofauti tofauti nchini Tanzania.Item Aina Tatu za Kahawa Tanzania(Mafatanzania blog/Mtanzania.co.tz, 2024-03) Matanzania blog, Mtanzania.co.tzKampuni ya ITO EN LTD, ambayo ni kampuni tanzu ya Tully’s Co. Ltd., inayomiliki migahawa maarufu ya Tully’s Coffee, imezindua aina tatu mpya za kahawa ya Tanzania, nchini Japan katika hafla iliyofayika jijini Tokyo tarehe 14 Machi, 2024. Aina za kinywaji hicho pendwa nchini humo kinachotokana na kahawa kutoka Tanzania ni TULLY’s COFFEE BARISTA BLACK KILIMANJARO; TULLY’S COFFEE MY HOME BLACK KILIMANJARO; na TULLY’S COFFEE BARISTA ROAST COLD BREW – KILIMANJARO BLEND. Kahawa hizo ni kutoka mkoa wa Arusha, Tarime mkoani mara na mashamba ya GDM yaliyoko Mbozi mkoani Mbeya.Item Mafunzo ya kilimo cha maharage(SUA, 2024-03) Chuo Kikuu cha kilimo cha Sokoine, Food LandKitabu hichi kimezungumzia mambo mbalimbali kama Maandalizi ya ardhi,namna bora ya upandaji, aina ya maharage na sifa zake na virutubisho vinavopatikana kwenye maharage.Item Kilimo Bora cha Migomba(Maendeleo Vijijini, 2017-03) Mbega, DanielKWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi, lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara.Item Kilimocha kunde(IIT, 2008-06) IIT, CGIARKunde ni zao jamii ya mikunde. Faida kubwa ya zao hili ni: • Chanzo cha viini lishe vya protini kwa binadamu na wanyama. • Mabaki ya mmea wa kunde ni chakula kizuri cha mifugo. • Hurutubisha udongo.Item Kilimo Cha Pamba Tanzania(Wauzaji Blog, 2024-08) Minja, LenaldKilimo cha Pamba hulimwa nchini Tanzania na hukuzwa mikoa mbalimbali na pia pamba ndio hutumika kutengenezea uzi na nguo,mafuta.Item Fahamu Kilimo Cha Njugu Mawe(Kilimoajira, 2018-09) KilimoajiraNjugu ni mbegu za mmea wa njugu. Mmea huo unapoendelea kusitawi huwa unachanua maua ya manjano ambayo hujichavusha yenyewe.Item Kilimo cha Matikiti Maji: Masoko na Fursa za Kibiashara(Mogri culture Tanzania, 2023-03) Mtalula, MohamedMatikiti maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi duniani zenye hali ya hewa ya joto la wastani. Zao hili lina wapatia watu shughuri za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Matikiti maji ni mojawapo ya jamii aina ya matunda au mbogaboga inayotambaa. Mimea hii inapatikana katika kundi linalojumuisha mimea mingine (curcubitaceae family) kama matango, maboga na maskwash (squash). Tikiti maji ni zao la kipekee ambalo limekuwa likibamba soko la ndani na nje ya Tanzania kutokana na ladha yake nzuri, faida zake kiafya, na matumizi yake katika viwanda vya chakula na vinywaji. Hata hivyo, ili kuweza kunufaika na soko hili, mkulima anahitaji kujua mbinu bora za kilimo, mahitaji ya soko, na fursa za biashara. Katika makala hii, nitaelezea kwa kina kuhusu masoko ya matikiti maji Tanzania, mahitaji ya soko, jinsi ya kuongeza uzalishaji, na fursa za biashara. Nitakupa miongozo na mikakati ya kufikia masoko ya ndani na nje ya nchi, na kujenga uhusiano mzuri na wanunuzi na wazalishaji wa viwandani. Kupitia makala hii, utajifunza jinsi ya kuongeza uzalishaji wa matikiti maji, jinsi ya kujenga thamani ya matunda yako, na jinsi ya kufikia masoko ya ndani na nje ya nchi. Kwa hiyo, endelea kusoma ili kuweza kujifunza zaidi kuhusu Kilimo cha tikiti Maji Tanzania na fursa zake za biashara.Item Faida za Kiafya zinazopatikana katika ulaji waTikitimaji(TUKO, 2022-05) TUKOUnapokula tikitimaji, utafaidi protini, Calcium, Phosphorus, Iron, Vitamin A, B6, C. Potasium, Magnesium, Carotene, mafuta, nyuzinyuzi (fiber), na madini mengineyo. Pia mwili utapata nguvu za kupambana na maradhi na kukuondoa katika hali hatari. Read more: https://kiswahili.tuko.co.ke/367173-faida-10-za-kiafya-zinazopatikana-katika-ulaji-wa-tikitimaji.htmlItem Kilimo cha Binzari(Wizara ya kilimo, 2014-01-31) Wizara ya kilimoJina la kitalaam ni Curcuma domestica na kwa kiingereza ni turmeric. Zao hili asili yake ni Mashariki ya Mbali, na linalimwa zaidi katika mkoa wa Tanga, Kagera Kilimanjaro, Morogoro naZanzibar.Item Kupanda Mikorosho mipya(Taasisi ya utafiti wa kilimo Naliendele, 2022-06-25) Taasisi ya utafiti wa kilimo NaliendeleKipeperushi kinazungumzia upandaji wa mikorosho mipya ambappo ni kitendo cha kuanzisha shamba jipya kwa kufuata kanuni za kilimo bora cha mikorosho.Mashamba ya wakulima wengi yana mavuno hafifu, uzaaji mdogo hali iliyotokana na upandaji holela na duni na utumiaji wa mbegu hafifu.Item Faida katika miradi ya kilimo - Maharage(Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, 2024-02-24) Mishili, Fulgence J.Kilimo Biashara ni shughuli za biashara na usimamizi zinazofanywa na makampuni na wazalishaji ambazo hujishughulisha katika utoaji wa pembejeo kwa sekta ya kilimo na ufugaji, kuzalisha mazao, uchakataji, usafirishaji, huduma za kifedha, usambazaji, au utafutaji wa masoko ya mazao.Item Matunzo ya Mikorosho shambani(Taasisi ya utafiti wa kilimo Naliendele, 2022-06-25) Taasisi ya utafiti wa kilimo NaliendeleItem Upogoleaji mikorosho michanga iliyobebeshwa(Taasisi ya utafiti wa kilimo Naliendele, 2022-06-25) Taasisi ya utafiti wa kilimo NaliendeleItem Uanzishwaji wa kitalu cha miche ya mikorosho.(Taasisi ya utafiti wa kilimo Naliendele, 2022-06-25) Taasisi ya utafiti wa kilimo NaliendeleItem Uanzishwaji wa kitalu cha miche ya mikorosho.(Taasisi ya utafiti wa kilimo Naliendele, 2022-06-25) Taasisi ya utafiti wa kilimo NaliendeleViriba vinaweza kutengenezwa kwa kutumia mifuko ya plastiki au karatasi ya plastiki kiuchumi viriba vidogo( i.e 7.5 sm kipenyo sm 20 kimo) Vinamanufaa zaidi kwasababu huhitaji udongo kidogo na huchukua eneo dogo la kitalu ukiringanisha na hivi vikubwa.Item Kilimo biashara, kilimo bora, mboga mboga na matunda(Mogri culture Tanzania, 2024-04-13) Mohamed, MtalulaKanuni hizi zinajumuisha Kuandaa shamba mapema, matumizi ya mbegu bora, Kupanda kwa wakati na kwa nafasi, matumizi bora ya maji, matumizi sahihi ya mbolea na viuatilifu, kudhibiti magugu, magonjwa na wadudu wa mazao. Pia matumizi ya zana bora za kilimo na teknolojia rafiki, utunzaji wa mazingira, kufuata kanuni za usalama na afya, na kufuata kanuni za uchumi. Makala hii inalenga kuwaelimisha wakulima juu ya umuhimu wa kanuni hizi na jinsi zinavyoweza kusaidia katika kuongeza uzalishaji wa mazao na kuboresha maisha yao na jamii kwa ujumla. Pia, inasisitiza umuhimu wa kuendelea kubuni na kutekeleza mbinu bora za kilimo ili kukabiliana na changamoto za sasa na za baadaye katika kilimo.Item Zao la Mahindi(Upscaling Technologies in Agriculture Through Knowledge and Extension, 2017-12) Farm RadioMwongozo huu ni matokeo ya mradi “Upscaling Technologies in Agriculture Through Knowledge and Extension (UPTAKE) katika mradi mkubwa wa “New Alliance ICT Extension Challenge Fund. UPTAKE unafadhiliwa na IFAD chini ya usimamizi wa Farm Radio International (FRI) na kutekelezwa na mashirika ya FRI na CABI. Mwongozo huu utasaidia kutoa mafunzo kwa maafisa ugani, wakulima na wadau mbalimbali katika uzalishaji wa mahindi. Mwongozo unaweza kutolewa nakala bure kama hautatumika kibiashara. Toleo hili limechapishwa mara ya pili kwa ufadhili wa IFAD.Item Faida za upandaji wa Mazao mbalimbali kwa njia ya mseto.(Farm radio fm, 2022-06-03) Karuga, JamesJinsi kulima baadhi ya mazao pamoja (kilimo mseto) kunaweza kuongeza mavuno. Ni mazao gani ambayo yanaweza kupandwa pamoja bila kuingilia ukuaji na ukomavu wa kila moja, kwa mfano mazao ya mahindi na mikunde. Pia kuna maelewano kati ya mahindi na kunde kwa sababu maharagwe yanazalisha naitrojeni na mahindi hutumia nitrojeni nyingi. Kwamba baadhi ya mimea au mazao, kwa mfano, spishi zinazofaa kwa kilimo mseto, zinaweza kupandwa pamoja na mazao ya mizabibu bila kuathiri ukuaji na ukomavu wao. Jinsi upandaji pamoja wa mazao na kuyachanganya pamoja unavyoweza kusaidia kuwafanya wakulima wadogo kuwa na uhakika wa chakula kwa kuwawezesha kuvuna zaidi ya zao moja na kuongeza mapato yao kwa kubadilisha fursa zao za soko. Faida za upandaji mazao mchanganyiko kwenye shamba moja kwenye kufunika udongo na kuongeza rutuba. Kwa mfano, wakati mmea kama mkunde unapopandwa kando ya mahindi, mimea mirefu ya mahindi hulinda maharagwe, huku maharagwe yakiweka naitrojeni kwenye udongo. Pia, mikunde yenye mizizi mirefu kama vile mbaazi inaweza kupenya kwenye ardhi ngumu, na kusaidia mizizi ya mahindi kupenya ndani ya udongo. Aina za miti ya kilimo mseto ambayo husaidia mazao kustawi bila kuingilia ukuaji wa mazao mengine.