Athari za mpango wa uthibitishaji wa kikundi wa FSC katika hali ya misitu na maisha ya jamii ndani ya hifadhi za misitu ya ardhi ya vijiji, wilaya ya kilwa, Tanzania.
Loading...
Date
2026-05
Authors
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
SUA
Abstract
Usimamizi wa Misitu Shirikishi unaotekelezwa na Jamii (Community Based Forest Management – CBFM) umeonekana kuwa nyenzo muhimu katika kuhamasisha usimamizi endelevu wa misitu pamoja na kuboresha maisha ya jamii zinazotegemea rasilimali za misitu.
Misitu iliyothibitishwa ilionyesha uboreshaji wa muundo wa misitu, kuongezeka kwa msongamano wa miti, eneo msingi kubwa zaidi pamoja na uoto mpya wenye afya ikilinganishwa na hali ilivyokuwa kabla ya uthibitishaji ,hali ya uoto mpya ilionesha uwepo mzuri wa miti michanga, huku mgawanyo wa kipenyo cha miti wenye umbo la “Inverse J-shaped” ukionesha uwepo wa mfumo imara na endelevu wa ikolojia ya misitu. Aidha, ongezeko la jamii za miti,viashiria vya ndege lilionesha kuwa uthibitishaji umechangia katika uhifadhi wa bioanuwai na kuboresha ubora wa makazi ndani ya hifadhi za misitu.
Description
Usimamizi wa Misitu Shirikishi unaotekelezwa na Jamii (Community Based Forest Management – CBFM) umeonekana kuwa nyenzo muhimu katika kuhamasisha usimamizi endelevu wa misitu pamoja na kuboresha maisha ya jamii zinazotegemea rasilimali za misitu.
Keywords
Citation
https://www.mkulima.ac.tz.