Jinsi ya kufanya kilimo cha Vitunguu Maji 2021
Loading...
Date
2016-06-11
Authors
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
mogriculture.com
Abstract
Kilimo cha vitunguu maji ni muhimu sana hapa Tanzania. Vitunguu vinaweza kutumika kama zao la chakula au la biashara kwa aina zote za wakulima, wakubwa na wadogo.
Zao la vitunguu linazalishwa kutokana na mbegu, na miche inakuzwa kwenye kitalu kabla ya kupandikizwa shambani. Miche inakuwa na ‘kuzaa’ vitunguu. Vitunguu vikikomaa, vinavunwa na kuuzwa au kuhifadhiwa ghalani.
Wingi na ubora wa mavuno hutegemea; hali ya hewa, aina ya vitunguu, aina ya mbegu bora, usimamizi wa kilimo bora, uangalizi wakati wa kuvuna, usafirishaji na uhifadhi bora. Mavuno ya vitunguu kwa ekari bado ni madogo sana hapa nchini (kiasi cha tani nne kwa ekari) na upotevu wa mazao baada ya kuvuna ni mkubwa (kiasi cha 50% – 80%) kutokana na uhifadhi duni.
Hivyo ukiwa kama mkulima unahitaji utaalamu wa kilimo bora cha vitunguu na njia bora za kuhifadhi ili kuongeza uzalishaji na kipato.
Description
Kilimo cha vitunguu maji
Keywords
Jinsi ya kufanya Kilimo cha Vitunguu Maji 2021
Citation
https://www.mogriculture.com/2016/06/kilimo-cha-vitunguu-maji/