Mpango wa matumizi bora ya ardhi ya vijiji: Mbinu ya mapinduzi ya kijani wilayani Mbarali, Mbeya

Loading...
Thumbnail Image

Date

2014-10

Authors

Journal Title

Journal ISSN

Volume Title

Publisher

EcoAgriculture

Abstract

Nchini Tanzania, mpango wa matumizi bora ya ardhi vijijini ulirasimishwa miaka ya hivi karibuni ikiwa ni moja ya mikakati katika mchakato wa kuleta maendeleo endelevu vijijini. Utekelezaji wa mpango huu hauna budi kuwa mikononi mwa wanavijiji wenyewe kwa kiasi kikubwa katika kugawa ardhi yao kwa matumizi mbalimbali ya kujikimu kimaisha kwa sasa na siku za baadaye na kuwa na uhifadhi endelevu wa mazingira. Maendeleo endelevu katika Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya yanaathiriwa na migogoro ya matumizi ya rasilimali ardhi na maji kwa muda mrefu sasa. Hii imetokana na uwezo wa ardhi kupungua kutoa mavuno ya kutosha na uhaba wa maji kwa matumizi mbalimbali hususan umwagiliaji, unyweshaji mifugo, uendelevu wa miminiko la maji kwenye bwawa la umeme, uhifadhi ya bionuai na mazingira. Mpango wa matumizi bora ya ardhi vijijini unasaidia kusimamia na utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi, maji na hifadhi ya mazingira.

Description

Keywords

Kilimo Salama, Kilimo Mazingira, Hifadhi ya mazingira, Ardhi

Citation