Chakula na Lishe
Permanent URI for this collection
Browse
Browsing Chakula na Lishe by Subject "Chakula"
Now showing 1 - 15 of 15
Results Per Page
Sort Options
Item Chakula dawa(Sokoine university of agriculture, 2022-10-22) Taasisi ya chakula na lisheChakula dawa ni chakula kilichotengenezwa na kurutubishwa kwa nishati,vitamin na madini.Chakula hiki kimetengenezwa ma mafuta na hakihitaji kuchanganywa na maji.Chakula dawa hutumika katika kutibu utapiamlo kwa sababu huwa kina nishati,vitamin na madini kiasi kikubwa.Item Chakula, lishe na saratani - vidokezo muhimu(COUNSENUTH, 2010-07)Saratani (Cancer) ni ugonjwa unaotokana na seli za mwili zilizopoteza mfumo wake wa kugawanyika na hivyo hazipo katika hali yake ya kawaida. Seli hizo huweza kugawanyika bila mpangilio maalum na kuharibu mkusanyiko wa seli nyingine. Seli za saratani hutokea sehemu moja ya mwili na zinaweza kusambaa sehemu nyingine za mwili kupitia mfumo wa damu na limfu (lymph). Saratani inaweza kuwa ya kurithi au kusababishwa na hali ya mazingira ya vitu mbalimbali kama vile ulaji wa vyakula vyenye visababisha saratani (carcinogenic compounds), km. nyama iliyochomwa mpaka kuungua kidogo, ulaji usio bora, pombe, uvutaji sigara au mionzi hatari, aina ya madini kama “asbestos” na “lead”. Zipo pia baadhi ya saratani zinazosababishwa na virusi kama vile saratani ya shingo ya kizazi.Item Jinsi ya kumlisha mtoto baada ya miezi sita(Quality Assurance Project - University Research Co., LLC, 2017)Kipeperushi kinachoelezea utaarishaji wa chakula kwa watoto wanaoanza kula kuanzia miezi sitaItem Kumbe! I can cook! Peace Corps / Tanzania Cookbook 2012(Peace Corps, 2012)In some ways, cooking is a metaphor for Peace Corps service. You try new things, and you fail. You experiment some more, and you succeed! Sometimes you ‘re really proud of what you’ve accomplished, and other times, you’d rather forget about it. What it really boils down to is being open to the possibilities and trying new things, and this cookbook can guide you along the way -- at least in the jikoni. This cookbook is meant as a guide, not as a rule. Nothing in here needs to be followed exactly as stated, and if you want to change or alter a recipe, be free! A wise old PCV once said “cook with your eyes, nose, and mouth.” It’s true! You’re the one eating the food, so make it the way you like it! Some of the recipes call for pretty safi things that are only available in regional centers or Dar. This isn’t meant to frustrate you, it’s meant to give you a few more options when you’re in Dar for medical and you want to cook up something for your ex-pat host. Or if you want to stock up on goodies while you’re there and feast for a few weeks when you get back to your site. Plus, you’ll probably take this cookbook back to America where you’ll have more tools than you need and all the ingredients you can imagine available at your fingertipsItem Mapishi Ya Mboga Za Asilia(AVRDC – The World Vegetable Center Regional Center for Africa, 2016)Kipeperushi kinachoelezea mapishi ya mboga mbalimbali za asili kwa ufupi.Item Mboga za watu wa Pwani - Kilifi Utamaduni Conservation Group(Bioversity International, 2011)Kitabu kinazungumzia mbogamboga za watu wa pwani ukanda wa Mombasa nchini Kenya na ikiwa ni kielelezo cha mboga zote za Kimijikenda. Mijikenda maana yake ni makabila tisa yanayosikilizana kwa lugha. Makabila hayo tisa ya Mijikenda ni Digo, Giryama, Kambe, Duruma, Rabai, Ribe, Jibana, Chonyi na Kauma.Item Mihogo inaweza kutumika kupunguza gharama ya juu ya chakula(Shirika la chakula duniani, 2022-05-22) Shirika la chakula DunianiKuna mboga kuu mbili za mizizi katika Afrika Magharibi - mihogo na viazi vikuu au magimbi. Muhogo unapatikana mwaka mzima, ni wa bei nafuu na unajulikana, au tukisema kwa usahihi, ulijulikana kuwa chakula cha maskini. Nyingine maarufu ni viazi vikuu, ambayo mwandishi wa Nigeria Chinua Achebe alitaja kama "mfalme wa mazao". Mavuno ya magimbi yanasubiriwa kwa hamu. Hakika, ibada maalum hufanywa kabla ya magimbi kuvunwa na kuliwa, na tunavaa nguo zetu bora zaidi ili kusherehekea zao hilo. Muhogo ni chakula bora cha kila siku na kilikuwa kama chakula cha kawaida cha maskini na watumishi. Ninaona kuwa Rais Yoweri Museveni wa Uganda anawataka watu wake kugeukia mlo wa mihogo kama dawa ya kuporomoka kwa bei ya ngano wakati huu ambapo gharama ya maisha duniani kote imepanda .Item Mwelekeo wa dunia katika kutegemea washawasha, senene na wadudu wengineo kama milo yenye virutubisho vingi(Shirika la chakula duniani, 2016-03-09) Shirika la chakula DunianiJe umewahi kufikiria kuwa wadudu lishe ni moja ya majawabu ya kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi, halikadhalika lishe na kutokomeza umaskini? Kama hapana, basi fuatilia makala hii kutoka mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo duniani, IFAD. Kilimo kinaongoza kwa kusababisha mabadiliko ya tabianchi na wakati huo huo ni sehemu ya majawabu ya kupunguza madhara ya mabadiliko ya tabianchi.Item Ninahitaji kiwango gani cha protini.(Shirika la chakula duniani, 2023-04-25) Shirika la chakula dunianiProtini ni nini? Protini ni moja ya virutubisho vitatu, pamoja na mafuta na wanga, ambayo tunahitaji kwa kiasi kikubwa (macro) katika mlo wetu. Nywele zetu, ngozi, mifupa na misuli yote yametengenezwa kutokana na protini tunazokula, kama vile vimeng'enya, homoni na viambata vya neurotransmitters ambavyo vina jukumu muhimu katika mwili. Protini huundwa na minyororo mirefu ya vitengo vidogo vinavyoitwa amino asidi. Vitalu hivi vya ujenzi hutumiwa katika mwili kwa ukuaji na ukarabati. Kuna asidi 20 za amino kwa jumla, tisa ambazo ni muhimu, ikimaanisha kuwa mwili hauwezi kuzitengeneza na lazima uzipate kwenye lishe. Vyakula vinavyotokana na wanyama, kama vile nyama na samaki, na baadhi ya vyanzo vya mimea - soya, quinoa, buckwheat na Quorn - vina asidi zote muhimu za amino, na kuzifanya kuwa vyanzo vya juu vya protini. Tunapokula vyakula hivi, vimeng'enya vyetu vya usagaji chakula huvigawanya katika vitengo vidogo vya asidi ya amino, ili viweze kutumiwa na mwili.Item Samaki wenye mafuta(Shirika la chakula duniani, 2022-03-09) Shirika la chakula Dunianisamaki wenye mafuta ni wazuri kwa afya? ikiwa ni hivyo, ni aina gani bora na unapaswa kula mara ngapi? Nicola Shubrook, mtaalamu wa lishe, anaelezea faida za samaki hawa.Samaki wa mafuta mengi ya asidi ya mafuta ya omega-3. Asidi ya mafuta ya Omega-3 inachukuliwa kuwa muhimu kwa mwili wa binadamu, hupatikana katika vyakula kwani haiwezi kuzalishwa na mwili.Item Tathmini ya Hali ya Lishe, Unasihi na Huduma za Lishe (NACS) - KITABU CHA MWEZESHAJI Mafunzo kwa Watoa Huduma katika Ngazi ya Jamii(Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, 2017)Lishe ina uhusiano mkubwa na afya. Lishe duni au utapiamlo unaotokana na ulaji duni na maradhi ni mojawapo ya matatizo makubwa ya afya nchini Tanzania. Utapiamlo unawaathiri zaidi watoto wenye umri chini ya miaka mitano na akina mama walio katika umri wa kuzaa hasa wajawazito na wanaonyonyesha. Utapiamlo kwa wanawake wajawazito na wanaonyonyesha unaweza kusababisha madhara ya muda mrefu kwa watoto wao. Pia, utapiamlo unahusishwa na magonjwa sugu kama vile kifua kikuu (TB) na UKIMWI, ambayo ni matatizo makuu hapa nchini Tanzania. Upungufu wa lishe katika kipindi cha miaka miwili (siku 1,000) ya mwanzo ya maisha ya mtoto unahusishwa na maradhi, vifo na uchelewaji wa ukuaji wa mwili na maendeleo ya akili. Upungufu huo unaweza kuathiri utendaji wa akili, matokeo ya uzazi, afya na tija ya kiuchumi wakati wa utu uzima. Watoto wachache tu wenye utapiamlo pamoja na watu wazima wametambuliwa na kutibiwa kwa kupitia vituo vya kutolea huduma ya afya. Lakini wengi wa watu hawa wakisha ruhusiwa toka vituo vya kutolea huduma ya afya baada ya kutibiwa utapiamlo huwa hawarejei tena kwa ajili ya ufuatiliaji. Watoa huduma katika ngazi ya jamii watasaidia katika kuimarisha utoaji wa huduma kati ya vituo vya kutolea huduma ya afya na jamii ili watu wenye utapiamlo waweze kutambuliwa, kutibiwa na kufuatiliwa mapema na hivyo kuboresha hali zao za lishe, kugundua dalili za utapiamlo mapema na kuepuka maambukizi. Shughuli hizi zitaimarisha mwendelezo wa utoaji wa huduma kati ya vituo vya kutolea huduma ya afya na jamii.Item UHUSIANO WA UHAKIKA WA CHAKULA, UKIMWI NA LISHE BORA: Warsha ilifanyika Makambako - Njombe Tarehe 30 Novemba - 04 Desemba 2004(TARP II-SUA Project, 2005-02) Lyimo, C. S; Malimbwi, R. E; Lyimo-Macha, J. G; Macha, E; Kawamala, PChuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) pamoja na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Norway (NLH) wakishirikiana na Wizara ya Kilimo na Chakula (MAFS), wamekuwa wakitekeleza mradi wa "Uhakika Wa Chakula na Pato la Kaya kwa Wakulima Wadogowadogo" (TARP II - SUA Project). Mradi ulianza mwaka 2000 na unagharamiwa na Serikali ya Norway pamoja na serikali ya Tanzania. Madhumuni ya warsha hii yanalenga kuleta ushirikiano wa karibu kati ya wakulima wadogo wadogo ngazi ya kaya, wagani, wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na watafiti wa kilimo na mipango katika kuinua uwezo wa maisha ya mtanzania katika ngazi ya kaya; kiuchumi, kiafya na maendeleo kwa ujumla. UKIMWI ni tatizo kubwa linatishia kuwepo kwa binadamu. UKIMWI hauishii kumuua muathirika na kupoteza nguvu kazi tu, lakini pia jamii ya muathirika huathirika kwa narnna moja au nyingine. Nguvu kazi ya muathirika hupotea kwa ajili ya kumuuguza mgonjwa; fedha nyingi hutumika kwani mgojwa anahitaji chakula maalum na dawa; watoto hukosa huduma ya wazazi na hivyo kushindwa kusoma au kupata lishe bora; mgonjwa anapofariki kuna gharama za mazishi na nguvu kazi-hupotea kuhudumia misiba. Warsha ililenga kubaini mtazamo wa jamii kuhusu athari za UKIMWI katika uhakika wa chakula na kukuza elimu ya UKIMWI na lishe bora kwa kutumia wataalamu walioshiriki.Item Upishi wa Samaki wa Maji Matamu(2013)Samaki ni aina moja ya chakula chenye manufaa zaidi ulimwenguni, huwa na manufaa ya kuotesha mwili kwa afya njema. Makusudi ya hiki kitabu ni kufahamisha manufaa na uzuri yanayoletwa na ulaji wa samaki. Cha nuia upishi sahihi wa samaki hiari na kukaanga kwa mafuta mengi ambao ni mtindo dhaifu kwa afya. Samaki sio wazuri kwa afya ya jamii nzima mbali inahitajika kwa wenye mahitaji speshali kwa familia kama kina mama wajawazito, watoto wachanga, wazee na hata wagonjwa.Item Viungo vya chakula(Shirika la chakula duniani, 2020-04-09) Shirika la chakula DunianiUtafiti mwingi juu ya pilipili umeonyesha namna pilipili inavyoweza kuathiri afya, lakini matokeo ni mchanganyiko Viungo kwenye chakula vimekuwa vikitumiwa kwa miaka mingi sana. Binzari' Turmeric' na pilipili zimefanyiwa utafiti katika miongo ya hivi karibuni... Lakini je huwa tunatumia viungo hivyo ipasavyo kwa ajili ya afya zetu au la?Na faida za viungo hivyo ni zile ambazo unahisi.Viungo vimekuwa sehemu ya milo yetu ya kila siku maelfu ya miaka ,tumezoea kula viazi vya kukaanga na pilipili, tangawizi kwenye chai na kuongeza kwenye mlo.Lakini hivi karibuni, baadhi ya viungo ambavyo vimekuwa vinatajwa kuwa tiba ya baadhi ya magonjwa ingawa hakuna tangazo rasmi linalothibitisha hoja hiyo.Binzari imekuwa ikitumika katika maeneo ya bara la Asia kwa millennia.Katika utafiti wa mwaka 2014 , haijawekwa wazi bado kuwa utumiaji wa viungo una faida za kiafyaItem Vyakula wanavyopaswa kula watoto(Shirika la chakula duniani, 2024-06-09) Williams, JoKama mzazi, mahitaji ya lishe ya mtoto wako mchanga na mtoto aliyekuwa kidogo ni wazi kuwa ni kipaumbele, na ni rahisi kuhisi kulemewa na habari nyingi za mitandaoni. Vyakula ambavyo mtoto hula katika miaka yao ya mapema vinaweza kuathiri tabia zao za ulaji baadaye maishani.Kwa hiyo ni muhimu kuanzisha uhusiano mzuri na chakula tangu umri mdogo. Mtoto wako anapoanza kula vyakula vigumu.Ili kuhakikisha mahitaji ya virutubishi ya mtoto wako yanatimia, unapaswa kuzingatia milo mitatu kwa siku. Milo hii inapaswa kujumuisha vyakula kutoka kila moja ya vikundi vitano vikuu vya chakula. Vyakula vya protini, kama vile samaki, nyama, mayai na kunde. Wanga, kama viazi na wali. Matunda na mboga za rangi tofauti. Maziwa na bidhaa za maziwa.