Mifugo na Uvuvi

Permanent URI for this collection

Browse

Recent Submissions

Now showing 1 - 20 of 140
  • Item
    Jarida la Mifugo na Uvuvi
    (Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025-04) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
    Serikali imekuwa ikichukua hatua na kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukabiliana na uvuvi haramu. Mikakati hiyo ni pamoja na kufanya maboresho ya Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo inayosimamia rasilimali za uvuvi ikiwemo matumizi ya teknolojia za kisasa katika kusimamia rasilimali za uvuvi, kuimarisha Vikundi vya Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi (BMUs), kutoa elimu ya kudhibiti uvuvi haramu na matumizi endelevu ya rasilimali za uvuvi, kuhamasisha uanzishwaji wa Vyama vya Ushirika wa Wavuvi na kuimarisha ufugaji wa viumbe maji.
  • Item
    Jarida la Mifugo na Uvuvi
    (Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025-02) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
    UVUVI NI UTAJIRI! ndivyo ambavyo unaweza kusema kupitia Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo inahakikisha inaleta mapinduzi makubwa katika Sekta ya Uvuvi kwa kuweka jicho la kipekee kwenye Uchumi wa Buluu. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatekeleza mradi wa ukopeshaji wa boti za kisasa kwa wavuvi wa Ukanda wa Pwani, Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa, ambapo mradi huo unalenga kuwezesha wananchi kufanya uvuvi na ukuzaji viumbe maji endelevu na wenye tija na kuwajengea mazingira wezeshi ili waweze kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi.
  • Item
    Jarida maalum la nanenane
    (Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
    Wizara ya mifugo na uvuvi imeibuka na ushindi huo baada ya kuongoza katika vigezo mbalimbali hali iliyochagizwa na maandalizi mazuri iliyofanya katika maonesho hayo huku kivutio kikubwa kikiwa ni Paredi ya Mifugo iliyoambatana na maonesho ya Ndege nyuki maalum inayotumika kwenye udhibiti wa Uvuvi haramu. Akizungumza katika kilele cha Maonesho hayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mbali na kuipongeza Wizara hiyo kwa jitihada ilizochukua katika udhibiti wa magonjwa ya Mifugo kupitia utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo, ameielekeza kuhakikisha inaweka kituo cha Ugani kwenye viwanja vya Maonesho hayo jijini Dodoma ambavyo rasmi leo vimetambulishwa kwa jina la Dkt. John Samwel Malecela ili wananchi waendelee kunufaika na elimu ya masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Mifugo na Uvuvi
  • Item
    Jarida maalum la chanjo ya Mifugo
    (Wizara ya Mifugo na uvuvi, 2025-08) Mbaraka Kambona; Edward Kondela; Elibariki Mafole; Hamisi Hussein; Omary Mtamike; Daudi Nyingo; Brayton Stanlay; Makwai Chiku
    Faida na Malengo ya chanjo na utambuzi . Chanjo ya Mifugo imelenga kulinda afya ya mifugo. .Kuongeza tija, kufungua masoko ya kimataifa kupitia diplomasia ya uchumi, na kuboresha kipato cha wafugaji. . Kupunguza gharama kwa ruzuku ya serikali na kutoa chanjo bure kwa baadhi ya mifugo.
  • Item
    Jarida maalum la nane nane 2025
    (Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2025) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amewataka viongozi wa sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi nchini kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha chakula katika ukanda wa Afrika. Mhe. Dkt. Mpango amesema hayo wakati wa hotuba yake ya Ufunguzi wa Maonesho ya kimataifa ya Nane Nane aliyoitoa Agosti 1, 2025 kwenye Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma ambapo amesisitiza Viongozi hao kuwa kinara kwenye utekelezaji wa dira ya Taifa Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025-2050. Aidha Dkt. Mpango amewataka wafugaji kuwekeza katika uzalishaji wa kisasa wa bidhaa zinazotokana na mifugo ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje, kuendeleza uvuvi na ufugaji wa samaki na kuvutia wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza kwenye miundombinu baridi ya uhifadhi na usafirishaji wa mazao wa Mifugo na Uvuvi.
  • Item
    Jarida la Mifugo na uvuvi
    (Wizara ya Mifugo na Uvuvi, 2026-01) Wizara ya Mifugo na Uvuvi
    Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ambapo wamejadili kuhusu miradi inayotekelezwa kuendeleza sekta ya mifugo na uvuvi. Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika Januari 16, 2026, ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameonesha kufurahishwa na ujio wa ujumbe huo ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa IFAD nchini. Amesema serikali ya awamu ya sita imeendelea kuimarisha mazingira rafiki ili kuruhusu wawekezaji na sekta binafsi kushiriki katika kusukuma maendeleo ya wananchi.
  • Item
    Bata mzinga
    (Ufugaji bora group, 2024-10-11) Ufugaji bora group
    Bata mzinga ni bata ambao wanahitaji matunzo ya hali ya juu. Kwa kawaida bata mzinga hula chakula kingi kuliko kuku. Bei yake ni ghali zaidi. Kabla ya kuanza ufugaji wa bata mzinga ni lazima kuhakikisha una chakula cha kutosha kwa sababu ulishaji wa ndege hawa kadri wanavyokua huwa na gharama kubwa zaidi.
  • Item
    Mwongozo wa ufugaji bora wa sungura
    (Wizara ya mifugo na uvuvi, 2020) Wizara ya mifugo na uvuvi
    Sungura wako katika kundi la mamalia wadogo katika familia ya Leporidae ya oda ya Lagomorpha .Kuna aina zaidi ya 45 za sungura duniani kote ambazo zinatofautiana kulingana na rangi ukubwa pamoja na matumizi.Sungura hutupatia nyama nyeupe isiyo na mafuta ya lehemu(cholesterol ) na hivyo wataalamu wa lishe huimiza nyama ya sungura kwani ni bora kwa afya hivyo kuitwa nyama tiba.
  • Item
    Mlo kamili wa kuku
    (Kuku site, 2024) Kuku site
    Mlo kamili wa kuku ni mlo wenye virutubisho vyote muhimu anavyohitaji kuku kwa kiwango na uwiano sahihi, Virutubisho vinavyohitajika katika mlo wa kuku ni kama ifuatavyo: 1.Wanga (carbohydrates) Wanga hutumika kama chanzo cha haraka cha nishati (nguvu) katika mwili wa kuku, na inapatikana katika nafaka mbalimbali kama Mahindi, Pumba ya mahindi, Ngano, Mtama, Mchele n.k 2. Protini ( protein ) Ni kirutubisho muhimu ambacho hujenga mwili. Protini inapatikana katika vyakula kama Mashudu ya Alizeti, Dagaa, Soya, Damu n.k 3.Mafuta (Fat) Mafuta ni muhimu sana katika lishe ya kuku kwani humuwezesha kuku kusharabu fat soluble vitamins kama vitamin A, D, E, na K, huhifadhi nishati, kutunza joto na kulinda ogani muhimu katika mwili wa kuku.
  • Item
    Malezi ya vifaranga
    (Kuku site, 2024) Kuku site
    Banda la vifaranga ni muhimu liandaliwe vizuri. Andaa banda/chumba (brooder room) utakachokitumia kwa ajili ya kulea vifaranga kiwe na sifa zifuatazo: • Hewa ya kutosha. • Mwanga wa kutosha • Chanzo cha joto kama vyungu vya joto au bulb zinazozalisha joto. • Mazingira rahisi ya kufanya usafi. • Nafasi ya kutosha kuepusha msongamano wa vifaranga.
  • Item
    Kitabu cha mafunzo kwa wafanyakazi wa afya ya wanyama
    (International Livestock Research Institute untranslated, 2018-07) International Livestock Research Institute
    Sungura na dende huitwa pia mara nyingi mafugo ndogondogo (mini-élevage). Kundi hili pia lina ndani na nyama zingine zinazo kula majani kama vile « Agoutis ». Sungura na dende zinakula majani, matunda na mbegu. Hizo ni nyama muhimu kwa malisho bora ya binadamu kwa watu wenyi pato ndogo wanaokumbwa na shida za udongo katika inchi nyingi duniani pote, hasa Amerika ya Kusini. Sababu kuu zinazo tuma sungura na dende za chaguliwa kama wanyama wakutowa nyama kwa matumizi ya jamaa na kwa soko ni: • Wao wanatowa kiasi kikubwa cha nyama yenyi onjo bora, tamu, safi na yenye malisho bora iliyo na proteini nyingi (hadi 21 %), yenyi kalori (ya kupana nguvu) chini, mafuta kidogo hasa ile mafuta mabaya yano itwa 3cholestérol » na chunvi ndogo. • Tofauti na wanyama wakubwa, kama vile nguruwe na mbuzi, sungura na dende zinaweza kutumiwa kwa kukuliwa limoja ndani ya jamaa bila kuyiweka siku nyingi ijapokuwa baridi ni shida. • Sungura na dende hujizidisha haraka. Ikiwa malisho yazo na matunzo ni bora, mufugaji ataweza anza ufogo na dike mbili (2) na dume moja (1) na ataweza eneza sungura makumi tano (50) ao zaidi ku mwaka. Hata wakati kuna chakula ya majani tu, dike tatu (3) na dume moja (1) wanaweza kutoa kilo 2 (2 Kg) cha nyama kwa juma na kuongeza chakula cha familia. Kwa upande mwingine, dike 50 hadi 150 hufanya kampuni (entreprise) kubwa ambayo hutoa kazi ku watu wengine na kuongeza pato ya zaidi. • Garama za chakula ni ndogo saana kwa sababu sungura na dende zinaweza kulishwa na majani mbalimbali, na kazalika. Sungura na dende zina tumbo sawa yenyi itaweza tumika sawa ngombe, farasi na tembo kuhusu chakula ya majani. • Sungura na dende zinatowa mboleo bora ambayo una vifaa mingi kuhusu malisho ya mimea hasa ma mbogamboga. Pia, mboleo ya sungura na dende ina proteini mingi, inaweza pia kukaushwa na kuongezwa ndani ya chakula cha wengine wa nyama sawa vile nguruwe, kuku, samaki na kazalika. • Sungura na dende ni rahisi kufuga, hata katika shamba ndogo au ndani za mijini. Nyumba za sungura na dende hazichukuwe nafasi kubwa na kwepesi kuzisafisha (sungura ni safi zaidi, kimya, dende kwa upande wake ni mchezaji mdogo). • Ngozi za sungura zina uzishwa. Kwa vile zinaweza tengeneza kofia, viato (pantouffles), na kazalika. Kwa kuendesha mradi mupya huyu wa ufugo ndogondogo ndani za jamaa inaitajika kuchunguza na kujuwa upendeleo ya wenyi watakao husika ila masuali za kiuchumi ni za maana sana. Jibu kuhusu swali la aina za wanyama wakufuga itazungumuzwa badaye kufwatana mambo itakayo zungumuzwa hapo chini. Ila ni muzuri kujuwa mbele kama siyo vema kufuga sungura dende fasi moja kwa sababu zina maitaji mbalimbali. Kampuni ya wanyama kutoka Ungereza inapendekeza: "Hatuna kupendekeza kuweka sungura na dende kwa sababu zina maitaji tafauti (kwa mfano chakula na nafasi). Sungura zinaweza kutisha dende, ambazo zinaweza kuzizuia ikiwa haziwezi kukimbia. Kuna pia vidudu sawa Bordetella bronchiseptica, inayopatikana katika sungura bila kuonyesha tatizo fulani ila itaweza leta shida za magonjwa za kifuwa/shida za kupumua kwa dende.
  • Item
    Sera ya Taifa ya ufugaji nyuki
    (KIUTA Dar es Salaam - Tanzania, 1998-03) Wizara ya maliasili na utalii
    Sekta ya ufugaji nyuki Tanzania imeendeshwa bila ya kuwa na sera tangu mwaka 1949 wakati ilipoanzishwa rasmi kama idara katika Wizara ya Kilimo. Tangu wakati huo, mwongozo wa kuendeleza na kusimamia rasilimali za nyuki na mimea ya chakula chao umekuwapo kupitia maagizo ya kitaalamu na kiutawala. Madhumuni makuu ya mwongozo huo yalikuwa ni kuufanya ufugaji wa nyuki uwe wa kisasa kwa kuanzisha mizinga ya masanduku, kuongeza uzalishaji wa asali na nta na kuongeza mapato yatokanayo na uuzaji wa asali na nta nchi za nje . Mabadiliko mengi ya kijamii, kiuchumi na kimazingira yanayotokea pamoja na marekebisho ya sera kuu ya uchumi yaliyotekelezwa nchini, na ongezeko la kujali uhifadhi wa mazingira ili kuleta maendeleo endelevu ya ufugaji nyuki yamepelekea kuundwa kwa Sera ya Ufugaji Nyuki. Sera hii inazingatia nafasi ya ushirikiano na uratibu wa sekta mtambuka ambao utaimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za nyuki na mimea ya chakula chao katika mashamba ya kilimo, misitu na maeneo ya wanyamapori yaliyohifadhiwa. Rasimu ya sera ya ufugaji nyuki awali ilitayarishwa kama sehemu ya Sera ya Misitu na utayarishaji wa rasimu hii ulihusisha washikadau husika katika warsha tatu tofauti, mikutano mbali mbali ya Idara ya Misitu na Nyuki, Washauri wa Kitaalamu na kikosi maalumu cha utekelezaji. Rasimu ya mwisho ilitayarishwa kwa kuboresha na kuunganisha hoja, mapendekezo na maazimio yaliyopitishwa na warsha hizo tatu na katika mikutano mingine ya kiushauri. Chanzo kingine muhimu cha habari zilizotumika katika rasimu hii ya mwisho ni Mpango wa Utekelezaji wa Misitu Tanzania (TFAP) ambao unajumuisha Programu ya Taifa ya Ufugaji Nyuki (NBP). Masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya sekta ya ufugaji nyuki yaliyokuwamo katika Programu ya Taifa ya Ufugaji Nyuki ambayo yalitayarishwa mwaka 1989 yakiwahusisha washikadau wakuu katika mikutano ya vijiji na warsha za kitaifa, yamejumuishwa katika sera hii. Iliamuliwa kuwa rasimu inayojitegemea ya Sera ya Ufugaji Nyuki iandikwe badala ya kuijumuisha na ile ya Misitu, ili malengo na madhumuni yake yawe bayana na yenye kueleweka. Hii pia inatazamiwa kuwa itawezesha kuzingatiwa kikamilifu kwa masuala ya sekta ya ufugaji nyuki na yale ya sekta mtambuka zenye misingi yake katika ufugaji nyuki na matamko ya sera ambayo ndiyo msingi wa uundaji wa Sheria ya Ufugaji Nyuki. Sheria ya Ufugaji Nyuki itakuwa ndiyo nyenzo kuu ya utekelezaji wa sera hii.
  • Item
    Ufugaji wa nyuki kibiashara na ubora wa mazao yake.
    (Wakala wa misitu Tanzania, 2019-05-02) Wakala wa misitu Tanzania
    Karne mbili zilizopita, ufugaji wa nyuki kibiashara ulianza baada ya kuibuka kwa teknolojia za kukabiliana na wadudu hao na kupanuka kwa soko la asali na mazao yake ikiwamo nta inayotumika viwandani. Licha ya kuwa na zaidi ya miaka 100 ukifanyika, bado biashara ya asali duniani ni fursa kwa wananchi, lakini wengi hawajui kama ipo na imekumbatia utajiri mkubwa. Tanzania ni nchi ya pili duniani katika uzalishaji asali; zao kuu litokanalo na nyuki ikiwa nyuma ya Ethiopia. Serikali kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), inaratibu shughuli za ufugaji wa nyuki na ushauri wa kibiashara kwa wazalishaji na wauzaji wa asali na mazao yake. Kalenda ya ufugaji wa nyuki nchini imegawanyika katika misimu minne kulingana na majira kwa mwaka, ambayo hutofautiana kati ya mkoa na mkoa. Kaimu meneja mawasiliano wa TFS, Tulizo Kilaga anasema katika kila msimu, kazi ya ufugaji wa nyuki hutegemea na kundi la nyuki linahitaji nini na mfugaji afanye nini kuweza kuzalisha mazao ya nyuki. “Ipo misimu minne ya nyuki kwa mwaka ambayo ni msimu wa njaa, kujijenga kwa nyuki, mtiririko wa asali na msimu wa mavuno kwa mfugaji wa nyuki,” anasema Kilaga.
  • Item
    Maua kwa wakulima na wafanyabiashara
    (Chuo cha kilimo cha Sokoine., 2009) Programu ya pantil
    Carnation’ ni ua ambalo asili yake ni nchi za Ulaya zenye hali ya hewa ya baridi. Hapa Tanzania maua ya ‘carnation’ yaliletwa na wazungu katika vipindi tofauti. Mpaka sasa maua haya yanalimwa vijiji vya Tchenzcma na Nyandira huko Mgeta na kijiji cha Ruvuma (Morning Side) mkoani Morogoro. Maua aina ya ‘carnation’ pia yanalimwa na kampuni ya Highlanders wilayani Njombe na kijiji cha Ndiwili wilayani Kilolo katika mkoa wa Iringa. Mpaka sasa ugavi wa maua ya ‘carnation’ hautoshelczi mahitaji ya soko la ndani. Kwa mfano, wafanyabiashara wanahitaji zaidi ya banchi 100,000 kwa mwaka wakati wakulima hawawezi hata kuzalisha nusu yake. Matokco yakc maua mengi ya ‘carnation’ kwa ajili ya soko la ndani hununuliwa toka Nairobi nchini Kenya. Ni dhahiri kuwa watu wengi nchini Tanzania hawajui kiliino cha maua ya ‘carnation’. Sehemu hii ya kijitabu ina lengo la kuelezea juu ya kilimo cha ‘carnation’ kwa wakulima wadogo wadogo. hasa uzalishaji wa michc, upandaji wa michc bustanini, utunzaji wa bustani na uvunaji wa maua.
  • Item
    Mwongozo wa kutengeneza chakula cha samaki na ulishaji wa samaki
    (Chuo cha kilimo cha Sokoine, 2022) Chuo kikuu cha kilimo cha sokoine
    Samaki kama viumbe hai wengine wanahitaji kula chakula ili waishi na kukua. Katika mazingira ya asili kama vile mito, maziwa na bahari, samaki hula chakula cha asili kinachopatikana ndani ya maji. Vyakula hivyo ni pamoja na jamii ya mimea na vijidudu wanaopatikana kwenye maji. Lakini, samaki wa kufugwa hususan ufugaji wa kibiashara, huhitaji kulishwa chakula cha ziada chenye ubora iliyo na virutubisho vinavyohitajika ili aweze kukua vyema na kwa haraka zaidi. Uandaaji wa chakula cha ziada cha samaki hutegemea zaidi aina ya samaki, mfumo wa samaki husika katika kumeng’enya (kusaga) chakula pamoja na kiasi cha virutubisho vinachohitajika.
  • Item
    Kuku wa kienyeji
    (Chuo cha kilimo cha Sokoine, 2002-12) TARP II SUA Project
    Warsha iliandaliwa na Mradi wa Uhakika wa Chakula na Pato la Kaya kwa Wakulima Wadogowadogo Tanzania (TARP II SUA) unaotekelezwa na Chuo Kikuu cha Sokoinc cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo na Chakula pamoja na Chuo Kikuu cha Norway cha Kilimo (NLH). Lcngo kuu la warsha lilikuwa ni kubaini sababu zinazofanya uzalishaji wa kuku wa kienyeji kutokidhi mahitaji ya soko na kubuni mbinu za kukabiliana nazo ili mkulima aweze kuongeza uzalishaji wa kuku wa kienyeji na anufaike na soko lililopo la kuku wa kienyeji. Warsha ilikuwa na madhumuni mahsusi yafuatayo ili kufanikisha lengo hilo.
  • Item
    Mafunzo ya ufugaji
    (inades formation Tanzania, 1992) Inades formation Tanzania
    Tanzania ina idadi kubwa ya kuku wa kienyeji wanaofugwa kwa mtindo wa huria vijijini na hata mijini. Katika mtindo huu wa ufugaji, kuku huachwa huru mchana kutwa kujitafutia chakula wao wenyewe. Pengine baadhi ya wakulima huwatupia kuku wao mabaki ya chakula, chenga za nafaka au nafaka zenyewe. Wapo pia wakulima walio na utaratibu wa kuwapa kuku wao pumba za nafaka na maji ya kunywa kila inapowezekana. Zinapofika nyakati za jioni kuku hulala jikoni, au ndani ya nyumba ya mkulima mwenyewe. Ingawaje ufugaji wa aina hii ni rahisi, lakini faida inayopaikana (kama ipo) ni ndogo sana. Kutokana na kuzaana wenyewe wa wenyewe (kutobadili jogoo), lishe duni n.k., kuku hawa wana umbo dogo. Hutaga mayai machache, tena madogo madogo. Nyama yao ina ladha nzuri, lakini kwa vile wana umbo dogo, kiasi cha nyama wanayotoa ni kidogo tu. Katika kijitabu hiki “Kufuga na Kuboresha Kuku wa Kienyeji” tutazungumzia jinsi ya kuboresha kuku wa kienyeji kwa njia ya uzalishaji, kutumia jogoo bora, kuboresha lishe ya kuku. Tutazungumzia pia njia mbalimbali za kufuga zinazoweza kumnufaisha mfugaji mdogo. Kutokana na maarifa haya wewe mkulima utaweza kuona haja ya kufanya mabadiliko katika ufugaji wako. Hi uweze kunufaika na ufugaji ni lazima uwe na mifugo bora. Kitabu hiki kimeandikwa ili kukupatia maarifa na mbinu za kutumia ili upate kuku bora kutokana na kuku wako wa kienyeji. Katika kitabu kingine “ Kufuga kuku wa biashara” Utajifunza maarifa na mbinu bora za ufugaji wa kuku wa biashara. Hawa ni kuku wa kigeni. Wanahitaji matunzo maalum tofauti na yale ya kuku wa kienyeji wanaoboreshwa.
  • Item
    Ngozi ni mali
    (chuo cha kilimo cha Sokoine, 2015) chuo kikuu cha kilimo cha sokoine
    Ngozi ni mail kwako wewe na kwa nchi yako. Ngozi za Tanganyika huuzwa mahali pote duniani. Ngozi za nchi yetu lazima ziwe safi kabisa ill ziweze knstahili sifa nzuri katika soko la dunia.
  • Item
    Kuanzia ngozi, nyama, maziwa na hata manyoya, ngamia ni lulu katika jamii
    (Shirika la chakula duniani, 2018-02) Shirika la chakula Duniani
    Ngamia ni mnyama muhimu katika maeneo ya ukame au baridi kali anakotumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo usafiri, chakula kupitia maziwa na nyama yake, kuwawezesha wanawake kiuchumi na pia kulinda mazingira. Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO limeutenga mwaka huu wa 2024 kuwa wa wanyama wa jamii ya ngamia ambao ni waokozi wa jamii za maeneo ya mbali katika zaidi ya mataifa 90.
  • Item
    Ufugaji wa kuku
    (Kituo cha mafunzo ya wakulima, 2023) SAT
    Mfugaji wa kuku ana jukumu la kuhakikisha kuku wake wanaishi katika mazingira mazuri kiasi cha kutosha kufanya uzalishaji.Kuku ni jamii ya ndege wanaofugwa.Vifaranga ni watoto wa kuku waliotoka kwenye yai wenyeumri kuanzia siku ya 0 mpaka miezi Kuku wanaokuwa: Hawa ni kuku waliotoka kwenye hatua ya vifaranga,umri ni miezi 2.5- 5.Kuku wakubwa ni kuku waliomaliza hatua ya kuku wanaokuwa,umri wao ni kuanzia miezi 5 na kuendelea.